Saturday, 27 December 2014

BREAKING NEWS:Ndege ya AirAsia yatoweka na abiria 160



 Ndege ya  AirAsia aina ya Airbus A320-200160 ikiwa na abiria imepoteza mawasiliano na vituo vya kuongozea ndege na haijulikani hatima yake.
Ndege hiyo ilikuwa inasafiri kutoka mji wa Indonesia wa Surabaya kwenda Singapore .
Imeelezwa kuwa mawasiliano ya mwisho na ndege hiyo iliyokuwa na mruko namba QZ8501 23:24 GMT.
Ndege hiyo ilitarajiwa kuwasili Singapore  saa 00:30 GMT.
Taarifa kutoka wizara ya uchukuzi inasema kwamba ndege hiyo ilipoteza mawasiliano wakati ikiwa bahari ya Javavya  kati ya visiwa vya Kalimantan na Java .
Ofisa mmoja kutoka wizara hiyo Hadi Mustofa alisema ndege hiyo kabla ya kupoteza mawasiliano iliomba kibali kupita njia ambayo si ya kawaida na anga lilikuwa na mawingu sana.

No comments:

Post a Comment